Unaambiwa utamu wa kazi huja pale unapoifanya kwa moyo na uwe unaipenda,haijalishi ni kazi gani. Unapowataja watu wanaovutia ,wanaojituma na kufanya kazi waipendayo kwa moyo, hutamsahau trafiki mmoja aliyepewa jina la "Magari".Ni katika jiji la Dar-es-Salaam,kwenye moja ya barabara kuu ndipo utakapomkuta trafiki huyu. hufanyakazi kwa mbwembwe na madoido ya hatari kwelikweli , huku akifurahi kiasi kwamba haonekani kuchoka . Tuige mfano wake ,ili kuleta maendeleo katika jamii na nchi kwa ujumla.
Hapa akiyachungulia magari kama bado yanakuja
Hapa akiyavuta magari kwa mbele
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni